Saturday, July 8, 2017

Hongera timu ya taifa ya Tanzania "Taifa Stars" kwa kuchukua nafasi ya 3 ya COSAFA

Tokeo la picha la tanzania flag
Picha: wikipedia

Hongera timu ya taifa ya Tanzania "Taifa Stars" kwa kushika nafasi ya 3 ya mashindano ya COSAFA nchini Afrika Kusini. Ushindi huo umekuja baada ya kuifunga Lesotho kwa mikwaju ya penati. Hakika wachezaji, benchi la ufundi na viongozi wa TFF chini ya Rais Jamal Malinzi mnastahili pongezi kwa hatua hii. Kipekee blogu hii inampongeza kocha Salum MAYANGA kwa kuiboresha timu ya Tanzania. Hakika, hivi sasa Tanzania inacheza soka zuri na la ushindani ukilinganisha na miaka ya nyuma. Hatua hii itainua Tanzania katika viwango wa FIFA na pia wachezaji watapata soko kimataifa. Aidha hatua hii imewafanya wachezaji kupata uzoefu na kuzoeana na hii itaiwezesha Tanzania kufanya vizuri katika michuano mingine ya kimataifa. 

No comments:

Post a Comment