Saturday, July 19, 2014

Hongera TFF kwa kuanza kuuza tiketi za mechi za soka kwa njia ya kieletroniki kati ya Taifa Stars na Timu ya Taifa ya Msumbiji

Hongera Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) kwa kuanza kuuza tiketi za mechi za soka kwa njia ya kieletroniki. Hakika blogu hii imefurahishwa sana na hatua hii ya maendeleo katika soka la Tanzania. Hivi karibuni TFF imetangaza kuuza tiketi za mchezo kati ya Timu ya Taifa ya Tanzania "Taifa stars" na Timu ya Taifa ya Msumbiji "Mambas" utakaofanyika jumapili 20 Julai 2014. 

Utaratibu huu licha ya kuboresha mapato yatokanayo na uuzaji tiketi nchini pia unawawezesha wapenzi wa soka kununua tiketi bila taabu. Ni simu yako ya mkononi ndiyo itakuwezesha kununua tiketi yako. 

Blogu hii inaomba utaratibu huu uwe wa kudumu na hasa kwa mechi za ligi kuu ya Tanzania Bara. Hongera sana TFF, Jamal Malinzi (Rais wa TFF), wajumbe wa kamati ya utendaji ya TFF, watendaji na wafanyakazi wa TFF, Max-Malipo na M-Pesa. Hakika maendeleo ya soka Tanzania yanawezekana!!

Ili kupata tiketi yako tumia M-PESA kwa kupiga *150*00# Kisha Bonyeza 4, Bonyeza tena 4 kisha weka Namba ya Kampuni 173399 Kisha Ingiza 7000 kama Namba ya Kumbukumbu ya Malipo, kisha andika tena 7000 kwenye Weka kiasi, Kisha weka namba ya siri na Baadaye bonyeza  1 Kukubali. Hapo utapokea ujumbe wenye orodha ya vituo vya MaxMalipo vya kuchukua tiketi ukiwa na namba ya uhakiki wa malipo yako.

Picha:tffnews.blogspot.com

No comments:

Post a Comment