Monday, July 7, 2014

Hongera VETA kwa kupata TUZO kwenye maonyesho ya 77 katika kipengele cha utoaji mafunzo na ujuzi

Hongera MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) kwa kupata TUZO kwenye maonyesho ya Sabasaba katika kipengele cha kundi la utoaji mafunzo pamoja na ujuzi nchini.
Hakika blogu hii imefurahishwa na juhudi za VETA katika kuwapa wananchi hasa vijana ujuzi ili kukabiliana na changamoto zilizopo nchini. Ujuzi wanaoupata vijana unawasaidia kuinua uchumi wa mtu moja moja na taifa kwa ujumla.
Blogu hii inaomba VETA izidi kutoa mafunzo mbalimbali kwa vijana na hasa walio katika mikoa na wilaya za pembezoni ili faida ya mafunzo iwe kwa taifa zima. Pia blogu hii inawaomba vijana bila ya kujali elimu walionayo kwa sasa kujiunga na vyuo vya VETA ili kupata ujuzi na maarifa ya kutenda kazi kivitendo. Nchi nyingi zilizoendelea na zinazoendelea zimetilia mkazo mafunzo ya namna hii "Vocational and Technical Education". Uwepo wa mafunzo ya namna hii huziwezesha nchi zilizoendelea na zinazoendelea kupata Nguvu Kazi yenye ujuzi na maarifa katika nyanja mbalimbali kama vile ufundi mchundo, ufundi makenika, ufundi uashi, ufundi bomba, watengeza vywele, wapaka rangi, mafundi wa kompyuta na magari, madereva wa magari makubwa kama matreka, maroli, waendesha mitambo na mashine kubwa, wahudumu wa hoteli, waongoza watalii nk.
Maendeleo ya taifa lolote yanakuwa shakani bila ya kuwa na watu wa namna hii katika nchi ambao wamepata mafunzo rasmi ya ufundi stadi katika nyanja mbalimbali.Mfano, huwezi jenga barabara zenye uhakika bila ya kuwa na watu waliopitia VETA katika fani ya ujenzi. Nchi yetu ina mafundi wengi sana ambao hawajapitia VETA, na hivyo ubora wa huduma zao kuwa hafifu. Pia taifa linapaswa kupitisha sheria kwa kazi za namna hii zifanywe na wale tu walioudhuria mafunzo ya namna hii na kufaulu. Unataka kujiunga na VETA? Bonyeza hapa.
Picha: veta.go.tz

No comments:

Post a Comment