Sunday, June 22, 2014

Hongera Mh Ummy Mwalimu kwa kutilia mkazo upandaji wa miti nchini

Hongera sana Mh Ummy Mwalimu kwa kutilia mkazo upandaji wa miti nchini. Mh Ummy ameshiriki katika upandaji miti Same mkoani Kilimanjaro katika kijiji cha Mabilioni tarehe 17/06/2014 ikiwa ni siku ya kupambana na hali ya jangwa na ukame duniani.

Upandaji miti una faida nyingi ikiwa ni pamoja na utunzaji mazingira ambapo kwa sasa ni suala la kimataifa. Upandaji wa miti pia unapendezesha manthari ya sehemu husika. Na mwisho miti huongeza pato la taifa kwa maana ya uvunaji na uuzaji wa mazao yatokanayo na miti kama mbao. Pia blogu hii imefurahishwa na mkakati wa kuhakikisha Halmashauri nchini zinatilia mkazo suala la upandaji miti. Pia blogu hii imefurahishwa suala la kuhamasisha makundi hasa ya vijana katika suala zima la upandaji miti.

Blogu hii inaomba licha ya juhudi za kupanda miti nchini pia kuwe na sheria na kanuni za kukata miti. Kuwa na utaratibu huu utaokoa miti mingi inayokatwa bila sababu ya msingi na hivyo kuharibu mazingira. Ipo mifano mingi ya watu kukata miti bila sababu za msingi. Kuwepo kwa sheria na kanuni kutawabana wale wote wanaofikiria kuharibu mazingira kwa kukata miti hovyo. Tanzania inaweza kuwa na sheria ama kanuni ya kama mtu ama kikundi kikitaka kukata mti lazima kiombe kibali (tunaweza kuanzia katika ofisi za mtaa/kijiji) ambazo zinatambuliwa na Halmashauri. Ni vizuri kukumbushana katika nchi zilizoendelea sio rahisi kukata mti ovyo LAZIMA uombe kibali toka mamlaka husika, hivyo Tanzania tuige mfano huo.


Blogu hii inaomba wadau wengine wa mazingira wamuunge mkono Mh Ummy katika jitihada za kupanda miti na kutunza mazingira.

Mh Ummy Mwalimu akipanda mti, katika kijiji cha Mabilioni, Same mkoani Kilimanjaro tarehe 17/06/2014

No comments:

Post a Comment