Monday, June 9, 2014

Hongera sana Mh Leticia Nyerere kwa kuwa mzalendo

Picha:parliament.go.tz - Mh Leticia Nyerere

Hongera sana Mh Leticia Nyerere kwa kuwa mzalendo. Hakika blogu hii imefurahishwa sana kwa jinsi alivyokuwa akichangia hoja ya kuridhia itifaki ya SADC fedha na uwekezaji katika bunge la bajeti linalofanyika Dodoma, Tanzania tarehe 06/06/2014. Mh Leticia amesikitishwa na jinsi watanzania wasivyo wazalendo, wanaoshabikia masuala ya ajabu ajabu. Amesikitishwa jinsi watanzania wasivyojivunia nchi yao na kuipenda. Ameshauri serikali iwaandae watanzania kushiriki katika jumuia hizi kama SADC na sio kuridhia tu. Watendaji wa serikali pamoja na watanzania wakiandaliwa vyema watakuwa washiriki wazuri katika SADC na kukuza uchumi wa nchi yetu. Pia watendaji wakiwa wazalendo nchi yetu itapata manufaa makubwa sana. Mh Leticia amesema watanzania wakiandaliwa na kushirikishwa kikamilifu, taifa litapiga hatua kubwa ya maendelo. Kwa kuridhia ya SADC fedha na uwekezaji, Tanzania itaweza kushirikiana na nchi nyingine katika kuwaletea wananchi wake maendeleo.

Tuwe WAZALENDO, ili tupige hatua kubwa ya maendeleo. Asante sana Mh Leticia Nyerere kwa kuwa mzalendo.


Hakika, blogu hii imekumbushwa maneno ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere miaka ya 60, “binadamu wote ni sawa na Afrika ni MOJA

No comments:

Post a Comment