Picha: bongo5.com
Picha: 24tanzania.com
Hongera Rais wa TFF, Jamal Malinzi na TFF kwa ujumla kwa kuipeleka Taifa Stars nchini Botswana kama sehemu ya mazoezi. Timu ya Taifa ya Tanzania inatarajiwa kuweka kambi ya mazoezi nchini Botswana kwa wiki mbili ikiwa ni maandalizi ya mechi dhidi ya Msumbiji. Taifa Stars inatarajiwa kupambana na Msumbiji Julai 20 mwaka huu 2014. Blogu hii inaamini haya ni maandalizi sahihi ya kiwango cha kimataifa ambayo kwa miaka mingi timu yetu iliyakosa. Hii mbali na kuwaandaa wachezaji vizuri inawapa motisha kubwa wachezaji. Wachezaji nao mbali ya kupata mazoezi stahili wanabaki na deni kwa watanzania na hivyo kucheza kwa kiwango kikubwa katika mechi ya mashindano.
Blogu hii inampongeza kwa dhati kabisa Rais wa TFF pamoja na TFF kwa ujumla kwa juhudi wanazo zionyesha katika kuisaidia Timu ya Taifa kusonga mbele na kufanya vizuri. Yapo mambo mengi ambayo TFF ya sasa imefanya ikiwa ni pamoja na kumleta kocha mzuri sana, Mholanzi Mart Nooij. Blogu hii inaomba TFF izidi kukuza mpira wa miguu nchini na hasa kwa kuangalia soka la vijana na watoto pamoja na kuhakikisha linapata mahitaji muhimu kama walimu bora, vifaa bora, viwanja bora, marefa bora, madaktari wa michezo bora, viongozi bora wa michezo kwa watoto pamoja kuwapa elimu ya darasani wakati wakiwa katika maboresho. Kazi hii inapaswa kufanywa na wadau wengine kama mashule, academy mbalimbali, wakati TFF inabaki kama mratibu na kuendesha mashindano. Kwa habari zaidi soma habari leo.
No comments:
Post a Comment