Monday, June 9, 2014

Hongera JK kwa kuliagiza Jeshi la Polisi kuwakamata wezi wa fedha za wakulima wa tumbaku mkoa wa Tabora

Picha:mwananchi.co.tz - Kilimo cha Tumbaku 
Hongera Rais Jakaya Kikwete kwa kuliagiza Jeshi la Polisi kuwakamata wezi wa fedha za wakulima wa tumbaku mkoa wa Tabora. Agizo hilo la Rais litawafanya wezi hao wakamatwe na kufikishwa mahakamani. Mh Rais alitoa agizo hilo wakati akizindua uchunguzi wa saratani ya mlango wa kizazi kwenye Viwanja vya Chipukizi, mkoani Tabora.
Hakika blogu hii imefurahishwa na kauli hii ya Rais ya kuwashughulikia wezi wa mali za umma hasa vyama vya ushirika nchini. Blogu hii inaamini vyama vya ushirika ndio msingi wa maendeleo kwa wakulima na wanaushirika nchini. Uimara wa vyama vya ushirika ndio uimara wa uchumi wa nchi yetu. Kinyume chake kama vyama vya ushirika vinashiriki katika matendo yasiyofaa, maendeleo ya wakulima, wanaushirika na wananchi kwa ujumla hayatakuwepo na hii itasababisha uchumi wetu kuyumba. Hii haikubaliki hata kidogo. 
Blogu hii inaomba vyombo vya dola vimulike vyama vyote nchini ili kama kuna wezi wa mali za wanaushirika ama wakulima washughulikiwe kikamilifu. Blogu hii inakumbuka miaka ya nyuma jinsi vyama vya ushirika vilivyoweza kuleta mchango mkubwa katika maendeleo nchini. Mfano mzuri wa zamani ni vyama vya ushirika mkoani Kilimanjaro na Kagera kupita zao la Kahawa. Vyama imara vya ushirika ndio msingi mkuu wa maendeleo ya nchi yetu ambapo sehemu kubwa ya wananchi ni wakulima.

No comments:

Post a Comment