Wednesday, June 11, 2014

Hongera kwa jamii ya Tanzania kwa ongezeko la UMRI wa KUISHI toka miaka 50 mpaka 60


Picha: mapsofworld.com
Hongera kwa serikali pamoja na jamii nzima ya Tanzania kwa ongezeko la UMRI wa KUISHI hapa TANZANIA. Kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012, umri wa kuishi kwa watanzania umeongezeka kutoka miaka 50 (sensa ya mwaka 1988) hadi kufikia miaka 61 (sensa ya mwaka 2012).

Hayo yalisemwa na mkurugenzi mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Dk Albina Chuwa wakati akiwasilisha taarifa za msingi za kidemografia, kijamii na kiuchumi kwenye hafla ya uzinduzi iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Aidha, alisema wanawake wanaishi umri mrefu zaidi kuliko wanaume. Matokeo haya yanaonyesha wastani wa umri wa kuishi kwa wanawake ni miaka 63 tofauti na wanaume ambao ni miaka 60. 

Ongezeko la umri wa kuishi limetokana na kukua kwa uchumi na kupungua kwa umaskini wa kipato miongoni mwa wananchi wa Tanzania. Aidha pia ongezeko hili linatokana na juhudi za serikali katika kuwaletea wananchi wake maendeleo na kutoa huduma za kijamii kama afya, elimu nk.

Blogu hii inaomba juhudi hizi ziimarishwe na serikali pamoja na wadau wengine wa maendeleo wa nchi hii ili umri angalao ufikie miaka 70 ya kuishi. Wadau wa maendeleo sio tu wale wanaotoa msaada mikubwa kwa taifa letu BALI hata yale mashirika yasiyo ya kiserikali nchini, taasisi na makampuni ya watu binafsi (mfano kuna hospitali na shule binafsi) nk. 

Kwa habari zaidi soma mwananchi.

No comments:

Post a Comment