Thursday, June 5, 2014

Hongera kamati ya Bunge kwa kuitaka TRA kutoa sharti kwa TFF kutumia tiketi za kieletroniki

Picha:parliament.go.tz - Mh Luhaga Joelson Mpina (Kisesa-CCM)
Hongera kamati ya Bunge ya Uchumi, Viwanda na Biashara kwa kwa kuitaka TRA (Mamlaka ya Mapato Tanzania) kutoa sharti kwa Chama Cha Mpira wa Miguu Nchini (TFF) kutumia mfumo wa tiketi za kieletroniki ili kuongeza mapato. Hayo yalisemwa na Mwenyekiti wa kamati hiyo Mh. Luhaga Joelson Mpina (Kisesa-CCM) kwenye bunge la bajeti mjini Dodoma.

Hakika blogu hii imefurahishwa sana na kauli hii ya Mh. Mpina wa kuitaka TRA iweke sharti kwa TFF ili kuongeza mapato. Aidha,kwa kutumia tiketi hizi za kieletroniki zitasaidia si tu kuongeza mapato ya nchi bali pia zitaongeza mapato ya vilabu pamoja na vyama vya soka vya mikoa na wilaya ikiwemo TFF yenyewe. Hii itaongeza uwazi miongoni mwa wadau wa soka nchini Tanzania. Pia matumizi ya tiketi hizi za kielektroniki yatapunguza hujuma na kuongeza hamasa kwa wavuja jasho (wachezaji).

Blogu hii inaomba kutoa takwimu zinazoonyesha uwezekano wa mapato kuhujumiwa na kukubaliana na hoja ya Mh. Mpina ya matumizi ya tiketi za kieletroniki. Blogu hii inakumbuka wakati timu ya taifa ya Tanzania, Taifa stars na Msumbiji zilipocheza mnamo septemba 2007 katika mchezo huo mapato yalikuwa zaidi ya milioni 600 (605,020,000)!!! Kulikuwa na hamasa na uwazi kupita kiasi LAKINI tangia wakati huo eti Tanzania haijawahi kupata mapato kama hayo!!!! ama yanayokaribia hayo!! na tena hata kabla ya mechi hiyo miaka yote ya nyuma hakujawahi kuwa na mapato kama hayo!!! Sasa ni zaidi ya miaka 6 tangu Tanzania icheze mechi ile kubwa katika uwanja huo lakini mapato yanayopatikana katika mechi zingine za kitaifa na kimataifa ni chini ya nusu ya mapato ya mechi ile ya ufunguzi wa uwanja wa mkuu wa taifa!!! Je, hii ni sawa???

Ndio maana blogu hii inaamini kuna hisia kwamba mapato ya mechi nyingi hupotea ama uliwa na wajanja HIVYO basi UTARATIBU huu utaweka UWAZI na serikali kupitia TRA kuchukua KODI halisi ili kujenga nchi yetu TANZANIA kupitia michezo hasa mchezo wa SOKA.



No comments:

Post a Comment