Saturday, June 14, 2014

Hongera Kikwete na Clouds Media kwa uzinduzi wa Tamasha la Uzalendo mjini Dodoma

Hongera Rais Kikwete na Clouds Media kwa uzinduzi wa Tamasha la Uzalendo mjini Dodoma. Tamasha hilo lilimezinduliwa rasmi na Mh Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dr Jakaya Mrisho Kikwete. Tamasha la Uzalendo ni jambo zuri sana na la kuungwa mkono na wazalendo na wananchi wa nchi hii kwa ujumla. Mbali na wasanii wa muziki wa kizazi kipya na Bongo MovieTamasha, pia Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda alikuwepo. Tamasha la Uzalendo lilienda pamoja na uzinduzi wa Video ya Wimbo Maalum wa Miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. 

Blogu hii imefurahishwa sana na uzinduzi wa Tamasha hili linaodumisha umoja, amani na upendo nchini. Uwepo wa upendo, amani na umoja ndio kichocheo cha maendeleo katika taifa lolote ikiwemo Tanzania. Asante Clouds Media, wasanii walioshiriki, wananchi walioshiriki pamoja na viongozi wakiongozwa na Mh Rais Kikwete.

Aidha lengo la jumla la tamasha hili ni kwa watanzania kudumisha uzalendo, upendo na kuithamini na kuipenda nchi yao. Helo helo watanzaniaaaa,Helo helo Upendoo wa kweli!

Picha:http://tanzaniatoday.co.tz/



No comments:

Post a Comment