Hongera Taifa Stars kwa kuitoa Timu ya Taifa ya Zimbabwe kwa jumla ya magoli 3 kwa 2. Hakika huo ni ushindi mzuri ambao watanzania wote wanajivunia. Blogu hii inaomba TFF kuiandaa mapema Timu yetu kabla ya kukutana na Timu ya Taifa ya Msumbiji. Tuna amini kwa juhudi zinazoonyeshwa na wachezaji na benchi la ufundi pamoja na shirikisho la mpira Tanzania (TFF), Timu yetu itasonga mbele kwa kuing'oa Timu ya Msumbiji. Timu ya Taifa ya Tanzania chini ya kocha wa Kiholanzi Mart Nooij inatarajiwa kuingia kambini jumatano ijayo. Blogu hii inaomba TFF kuhakikisha Timu yetu inapata mechi mbili za kimataifa za maandalizi kabla ya kupambana na Msumbiji. Blogu hii inawaomba wadau wasibweteke na ushindi na wajue ushindi ulipatikana kutokana na maandalizi mazuri pamoja na mechi za majaribio za kimataifa (Burundi na Malawi mara mbili). Ukiangalia hapo hizo zilikuwa mechi 3, ya kwanza tulifungwa ila ya mwisho tukashinda dhidi ya Malawi. Kwa hiyo ushindi haukuja kiwepesi ila ni kutokana na mipango, maandalizi na mechi za kimataifa za majaribio. Hivyo, blogu hii inasisitiza maandalizi na mechi za majaribio kabla ya kukutana na Msumbiji.
Picha: bongo5.com
No comments:
Post a Comment