Hongera Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) kwa kuboresha huduma za ndege. Hakika blogu hii imefurahishwa na maboresho ya huduma za ndege hapa nchini. Shirika la ndege katika siku za karibuni limeongeza huduma zake katika mikoa mbalimbali nchini Tanzania na nje ya nchi. Kwa uchache kuna usafiri wa ndege kupitia ATCL Dar - Mwanza - Dar, Dar - Kigoma - Dar, Dar - Mbeya - Dar, Dar - Mtwara - Dar, Dar - Mbeya - Dar, Dar - Bujumbura - Dar, Arusha - Zanzibar - Arusha nk.
Shirika hili ni la taifa, hivyo basi kama wazalendo wa nchi hii hatuna budi kuipongeza serikali ya Tanzania kupitia Waziri wa Uchukuzi Mh Dr. Harrison Mwakyembe kwa juhudi za kuboresha huduma na usafiri kupitia shirika letu la taifa. Pia blogu hii inawapongeza manejimenti na wafanyakazi wa ATCL kwa ujumla kwa juhudi wazifanyazo ambazo zimeonyesha matunda haya. Tanzania ni nchi kubwa na inastahili kuwa na shirika bora la umma la ndege. Si ni a ya blogu hii kuonyesha mafanikio ya mashirika ya ndege ya nchi nyingine barani Afrika BALI Tanzania tunapaswa kuwafikia na kuwazidi wengine (nchi nyingine za Afrika). Kwa habari zaidi tembelea ATCL ili ujionee mwenyewe. Mwenye MACHO AAMBIWI TAZAMA.
Picha: http://www.mwananchi.co.tz

No comments:
Post a Comment