Thursday, May 22, 2014

Hongera serikali kwa kujali njia za mchepuko katika kupunguza msongamano magari jijini Dar es Salaam

Hongera Wizara ya Ujenzi kwa kutenga jumla ya Tshs 28.94 bilioni kwa ajili ya miradi ya ujenzi wa barabara za mchepuko ili kupunguza msongamano wa magari jijini Dar es Salaam. Pia blogu hii inapenda kumpongeza Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi John Pombe Magufuli kwa utendaji uliotukuka wa ujenzi wa barabara ndani ya jiji la Dar es Salaam na nchini kwa ujumla. Kiasi cha Tshs 28.94 bilioni zitatumika katika kupanua baadhi ya barabara, kukarabati baadhi ya barabara na kujenga barabara mpya kwa kiwango cha lami jijini Dar es Salaam. Hakika blogu hii imefurahishwa na hatua hii ya serikali ya kuhakikisha inapunguza msingamano wa magari katika njia kuu za magari jijini Dar es Salaam. Msongamano wa magari jijini Dar es Salaam licha ya kuwafanya wakazi jiji la Dar es Salaam kupoteza muda mwingi barabarani bali Taifa linapoteza pato kubwa.

Blogu hii inaomba hatua hii nzuri ya serikali isihishie katika barabara kumi bali iendelee kwa barabara nyingine kama vile barabara toka Mwananyamala Hospitali kuelekea kituo kipya cha daladala cha Makumbusho kuelekea Mwenge kupitia nyuma ya Jengo la Sayansi "COSTECH" mpaka makutano ya barabara ya Shekilango. Blogu hii ingependa mara barabara hii ikikamilika basi magari toka Mwananyamala Hospital mpaka Mwenge yapite njia hiyo ili kupunguza msongamano. 

Pia blogu hii inaomba hatua hii isiishie Dar es Salaam pekee bali hata mikoa mingine kama vile Arusha, Mwanza, Tanga, Mbeya nk inahitaji njia za michepuko ili kukabiliana na msongamano wa magari siku za usoni. Kwa habari zaidi soma mwananchi.

Picha:globalpublishers.info

No comments:

Post a Comment