Mojawapo ya taarifa zilizowafurahisha wafanyakazi
hapa nchini ni uamuzi wa wa serikali ya Tanzania kuwapunguzia wafanyakazi kodi wanayotozwa
kila mwezi kwenye mishahara yao. Makato ya kodi mpaka sasa kwenye mishahara ya
wafanyakazi ni asilimia 13. Kuna uwezekano mkubwa kwa kodi hii kupungua na kuwa
chini ya asilimia 10.
Katika siku ya MEI MOSI jijini Dar es Salaam, Rais Jakaya Kikwete aliliambia
taifa kuwa utekelezaji wa kupunguza kodi utaanza baada ya kupitishwa kwa bajeti
ya mwaka ujao. Lengo kuu likiwa ni kuwapunguzia wafanyakazi mzigo wa kodi na
kuwapa unafuu wa maisha.
Hakika blogu hii imefurahishwa na hatua ya
serikali kupitia kwa Mh Rais Jakaya Kikwete kupunguza kodi kwa wafanyakazi.
Wafanyakazi wa Tanzania wanakabiliwa na changamoto za maisha hivyo kwa
kuwapunguzia kodi ya PAYE (Pay as You Earn) kutawawezesha wafanyakazi kupata
nafuu katika maisha yao ya kila siku. Baadhi ya wafanyakazi kama vile walimu
watafaidika sana na punguzo hili, hali hii itaongeza motisha katika utendaji
wao wa kazi na matokeo yake watoto wetu watapata elimu bora kupitia kwa walimu
wenye motisha.
Aidha blogu hii bado inaipongeza serikali kwa
hatua zake za kupunguza kodi hii mwaka hadi mwaka. Mfano mwaka 2007, kodi hii
ilikuwa kiasi cha asilimia 18 na ikashuka na kufika asilimia 13. Sasa kuna
uwezekano kodi kuwa chini ya asilimia 10.Ni matumaini ya blogu hii punguzo hili la kodi
kwa wafanyakazi litafidiwa na serikali kupitia vyanzo vingine ili uchumi wa
nchi usiyumbe.
Mwisho, blogu hii inawaomba wafanyakazi na hasa
walimu kujiunga katika vikundi kama vile saccos, vikoba nk ili kuinua vipatao
vyao kwa maana hakuna mshahara unaotosha!! Kwenye vikoba na saccos wanaweza
kupata manufaa mengi sana ikiwemo kuwa na uwezo wa kujenga nyumba za kuishi.
Picha: fullshangweblog.com
Picha: farmlandgrab.org
No comments:
Post a Comment