Sunday, August 24, 2014

Hongera Rais Kikwete kwa kuahidi kuboresha sekta ya huduma ya afya kwa njia ya mtandao


Image result for kikwete
Picha: en.wikiquote.org     

Picha: ippmedia.com

Hongera Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Jakaya Mrisho Kikwete, kwa kuahidi kuboresha sekta ya huduma ya afya kwa njia ya mtandao.

Rais alisema hayo wakati akizungumza na wananchi wa vijiji vya Kisaki, Matombo, Dutumi na Kinole Morogoro vijijini. Aidha alisema huduma itakayotolewa itapunguza vifo vya wagonjwa hasa akina mama wajawazito na watoto.

Huduma ya matibabu kwa njia ya mtandao itafanya mawasiliano ya moja kwa moja kutoka kwa madaktari bingwa wa ndani na nje ya nchi wakati wa kutoa matibabu. Aidha, huduma ya mtandao imeonyesha mafanikio makubwa  kwa madaktari wa ngazi ya chini kuwasiliana na madaktari bingwa popote duniani na kuokoa maisha ya mgonjwa.

Blogu hii inaomba huduma hii itolewe nchi nzima hasa maeneo ya vijijini. Blogu hii inasisitiza kuwa kutokana na maendeleo ya teknolojia hasa ya simu na internet inawezekana huduma ya namna hii kutolewa bila tatizo lolote. 

Ni rahisi kutoa visingizio kuwa baadhi ya vijiji nchini havina umeme wa kuchajia simu na vifaa vya kielektroniki. Lakini huduma za solar, betri za magari makubwa, pamoja na booster charger za kisasa zinasaidia katika kupatikana kwa nishati. Suala linalotakiwa ni kwa Wizara ya Afya pamoja na halmashauri za miji na mikoa kujipanga katika kufanikisha huduma ya afya kwa njia ya mtandao ili kuokoa maisha ya watanzania hasa wakina mama na watoto. 

No comments:

Post a Comment