Thursday, February 12, 2015

Asante Waziri mpya wa Nishati na Madini Mh. George Simbachawene kwa kuwajali watanzania “kushuka kwa bei ya mafuta kuonekane kwenye huduma zingine pia”

Image result for simbachawene
Mheshimiwa George Simbachawene, Waziri wa Nishati na Madini
(Picha: parliament.go.tz)
Hakika blogu hii inakupongeza kwa kauli madhubuti ya kutaka kushuka kwa bei ya mafuta duniani na nchini kuonekane kwenye huduma nyingine pia. Mh. George Simbachawene alienda mbali na kusema kama mafuta nchini yameshuka kwa kiasi cha Tshs 180 kwa lita ni vyema hata huduma zingine kama za usafirishaji zishuke kwa kiwango hicho pia. Ametoa changamoto kwa wasimamizi kama SUMATRA kuangalia namna ya kufanya ili punguzo hili la mafuta lionekane kwa watu wa chini pia. 

Mh alienda mbali zaidi na sisi kama wanablogu ya “tuijengetanzania” tunakubaliana naye, kuwa kama lita moja imepungua kwa Tshs 180 inapelekea mtoa huduma kupata nafuu ya Tshs 60,000/= kwa kiwango cha chini kwa mwezi, hivyo punguzo hilo linatakiwa lionekane kwa abiria wanaolipa nauli za daladala kwa mfano au wanaokwenda na kutoka mikoani.

Pia TANESCO, kwa kuwa kwa kiasi bado wanategemea uzalishaji kwa kutumia mafuta basi pia wampunguze kiwango hicho kidogo kilichopungua hata kama ni 0.001 kwa mtumiaji wa mwisho wa umeme. Kuna wasafirishaji wa mazao toka mikoani kwenda kwenye miji mikubwa kama Dar es Salaam, Arusha nk, nao pia wapunguze gharama kwa wateja ili punguzo la bei ya mafuta liweze kuonekana kwa mtu wa mwisho.

Blogu hii inasumbuliwa na utamaduni wa kupenda kupandisha huduma mara baada ya mafuta kupanda, lakini inakuwa ngumu kushusha huduma zingine mara mafuta yanaposhuka.

Asante Mh. Simbachawene, na ni matumaini ya blogu hii wasimamizi wengine kama SUMATRA watasikia wito wako. Hakika nimeipenda hii “kama kupanda kwa mafuta vipande vyote, kama kushuka kwa mafuta vishuke vyote”. Big up Mh Simbachawene

No comments:

Post a Comment