Hakika blogu hii inawapongeza kwa
dhati kwa namna mlivyomjali Mama wa mtoto aliyetekwa na kuuwawa kikatili . Mtoto (Yohana Bahati) huyo mwenye umri wa mwaka mmoja alikuwa mlemavu wa ngozi mwenye “albinism”. Mama wa mtoto huyo baada ya kujeruhiwa wakati akipambana na watu waliomteka na kumuua mwanae amelazwa katika hospitali ya Bugando, mjini Mwanza. Msaada wenu wa shilingi milioni moja sio mdogo. Blogu hii inawapongeza sana na
inawaomba mzidi kuwasaidia watu maskini na wenye mahitaji maalum.
Pia blogu hii inaomba viongozi na
wadau wengine wajitokeze kusaidia katika mapambano dhidi ya ukatili kwa watu
wenye ulemavu wa ngozi. Pia blogu hii inaomba serikali kupitia vyombo vyake
ifanye “operation” kama ilivyofanya Tanga wakati ikipambana na watu waliokuwa
wanasadikiwa ni majambazi ama magaidi. Pia kuwepo na mahakama maalumu ya kushugulikia
kesi za watu wanaoua watu wenye ulemavu wa ngozi.
Picha: sundayshomari.com
Picha: thehabari.com
No comments:
Post a Comment