
Picha: africanleadership.co.uk
Hongera Mh John Pombe MAGUFULI kwa kuchaguliwa na wananchi wa Tanzania kwa kura nyingi. Hakika watanzania wamekuamini na kukupa kura kwa matarajio makubwa sana. Ni matumaini ya Blogu hii kuwa utawaletea watanzania wote maendeleo ya dhati. Hakika Blogu hii inaamini imepata si tu RAIS bali mlinzi na mtetezi wa wanyonge. Mwenyezi MUNGU akubariki na kukulinda.
Aidha Blogu hii inawakumbusha watanzania kuwa katika uchaguzi kunakuwa na ushindani mkubwa wa pande mbalimbali zinazotaka kuongoza nchi LAKINI akishapatikana MSHINDI ni jukumu la wote kushirikiana kuijenga nchi kwa UAMINIFU na WELEDI mkubwa.
No comments:
Post a Comment