Hongera Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kupitia kwa Mkurugenzi wake Mkuu Ndugu Nehemiah Kyando Mchechu kwa ujenzi wa makazi bora kabisa nchini. Hakika nchi hii inahitaji watu wenye akili, ujasiri na uthubutu kama wewe. Blogu hii inakutakia kila la kheri wewe na manejimenti nzima ya NHC katika ujenzi wa makazi bora. Ombi la blogu hii ni kuomba kwa kadri itakavyowezekana zijengwe nyumba za bei nafuu kwa wananchi wa kawaida. Na pia NHC iangalie uwezekano wa kuwakopesha watumishi wa umma nyumba kwa mikopo ya muda mrefu kama miaka 30+.

No comments:
Post a Comment