
Picha: Habari leo
Hongera Mh. Dkt. Jakaya Kikwete kwa kuzindua Taasisi ya MOYO ya Jakaya Kikwete jijini Dar es Salaam. Kupitia Taasisi hii Serikali itakuwa ikiokoa TShs Bilioni 2.5 kwa mwaka kutokana na upelekaji wa wagonjwa nje ya nchi.
Blogu hii inampongeza sana JK na serikali kwa ujumla kupitia wizara ya afya kwa uzinduzi wa taasisi hii ya kisasa ya magonjwa ya moyo katika ukanda wa Afrika Mashariki. Blogu hii inaomba jengo na vitendea kazi vitunzwe ili lengo la serikali likamilike. Aidha blogu hii inaishukuru serikali ya China kwa kutoa msaada wa Tshs Bilioni 16.6 katika ujenzi wa jengo la taasisi hii kutokana na jitihada zilizofanywa na Rais Kikwete alipotembelea China na kukutana na Rais Hu Jintao.
No comments:
Post a Comment