Monday, September 14, 2015

Hongera Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kuahidi kushirikiana na sekta binafsi katika kuboresha miundombinu ya Utalii nchini

Picha:Wizara ya Maliasili na Utalii

Hongera Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kuahidi kushirikiana na sekta binafsi katika kuboresha miundombinu ya Utalii nchini kwa kusudi ya kuwavutia watalii wengi zaidi kutembelea vivutio vingi vya utalii vilivyopo Tanzania. Miundombinu kama barabara zimekuwa katika hali mbaya na kukwamisha jitihada za serikali kuongeza watalii nchini.

Akizungumza katika mkutano wa sita wa Uchumi wa Tanzania ulioandaliwa na Benki ya Dunia katika Hoteli ya Kilimanjaro jijini Dar es Salaam, Rais Mstaafu wa Tanzania Mh Benjamini Mkapa alisema ni lazima sekta binafsi ishirikiane na Serikali badala ya Serikali kufanya kila kitu. SERIKALI HAIWEZI KUFANYA KILA KITU HIVYO SEKTA BINAFSI LAZIMA ISHIRIKISHWE KATIKA KUINUA UCHUMI.

Blogu hii imefurahishwa na Wizara ya Maliasili na Utalii ya kukubali kushirikiana na sekta binafsi katika kukuza sekta hii muhimu nchini kwa ustawi wa taifa letu. Pia blogu hii inawaomba watanzania na hasa wawekezaji wa ndani kuchangamkia fursa hii ili kujipatia kipato na kuinua pato la taifa.

Kwa habari zaidi, bofya hapa.

No comments:

Post a Comment