Saturday, September 12, 2015

Hongera Taifa stars kwa kuionyesha dunia kuwa mnaweza


Picha: Mwananchi.co.tz

Hongera Taifa stars kwa kuonyesha dunia kuwa mnaweza katika mechi kati ya Tanzania "Taifa stars" na Nigeria "Green Eagles" iliyochezwa jijini Dar es Salaam. Mechi hiyo iliyochezwa Septemba 5 2015 kuwania tiketi ya kufuzu AFCON 2017. Hakika wachezaji wamecheza kwa bidii sana wakiongozwa na Mbwana Samatta na Haji Mwinyi. Hakika kila mchezaji ameonyesha kiwango kikubwa. Haikuwa rahisi kuona tofauti ya kiuchezaji kati ya wachezaji wa kulipwa wa Nigeria na wale wanaocheza ligi ya ndani ya Tanzania. Benchi la ufundi nalo linastahili pongezi za dhati likiongozwa na Charles Boniface Mkwassa aka "Master" na Abdallah "King" Kibadeni aka "Mputa". Aidha blogu hii inaipongeza TFF kwa jitihada ilizofanya za kuibadili timu hii. Blogu hii inaomba juhudi hizo ziendelezwe. Pia blogu hii inaiomba serikali izidi kushirikiana na TFF katika kuisaidia timu ya Taifa. 

No comments:

Post a Comment