Sunday, December 13, 2015

Hongera Mawaziri na Manaibu Waziri kwa kuteuliwa na Mh Rais Dr MAGUFULI

Rais John Magufuli akisalimiana kwa furaha na wanahabari mara baada ya kutangaza baraza lake la mawaziri, Ikulu Dar es Salaam jana. (Picha na Ikulu).
Picha: Rais Magufuli akisalimiana na wanahabari baada ya kutangaza Baraza jipya la Mawaziri Ikulu jijini Dar es Salaam
 (source:habarileo)

Hongera baadhi ya watanzania wachache mlioteuliwa na Mh Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli kuwa Mawaziri na Manaibu Waziri wa Wizara mbalimbali. Hakika Mh Rais kawaamini sana na ana matarajio makubwa kuwa mtatenda kazi kwa uaminifu, uadilifu, na uweledi wa hali ya juu. Vile vile wananchi wa Tanzania wana matarajio makubwa na nyinyi wateule ukizingatia kasi nzuri ya Mh Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu. Jumamosi ya tarehe 12/12/2015 wataule mmeapishwa kwa kura kiapo. Kiapo kina maana kubwa sana kwenu binafsi, kwa Rais na kwa wananchi wa Tanzania. Blogu hii inamwomba Mwenyezi Mungu awaongoze katika utendaji wenu. Wananchi wengi wamefurahia uteuzi wenu kama inavyoonekana kwenye vyombo mbalimbali vya habari, mfano habari leo.

Blogu hii inawapongeza sana kwa kuteuliwa na inawaomba mchape kazi usiku na mchana ili Tanzania isonge mbele kijamii, kiuchumi na kisiasa kwa mtu mmoja mmoja na kwa taifa kwa jumla. 

No comments:

Post a Comment