
Picha:taarifa.co.tz
Hongera Mh Paul Makonda Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni kwa kufanikisha jambo zuri sana la walimu jijini Dar es Salaam kusafiri bure ndani ya daladala. Kuanzia tarehe 07 Machi 2016 walimu wote wa shule za msingi na sekondari jijini Dar es Salaam hawatalipa nauli za daladala. Hakika blogu hii imefurahishwa sana na kiongozi huyu kijana ambaye amefanya jambo zuri nchini. Blogu hii inawapongeza pia viongozi wa wenye mabasi ya daladala kwa kukubaliana na wazo la Mkuu wa Wilaya. Hakika walimu ni watu muhimu sana katika taifa lolote, hususan Tanzania. Blogu hii inaomba viongozi wengine waige ubunifu kama wa Mkuu huyu wa Wilaya ya Kinondoni.
No comments:
Post a Comment