Wednesday, April 20, 2016

Hongera Dr John Pombe Magufuli kwa kuzindua daraja la kigamboni

Picha: teamtz.com
Hongera Dr John Pombe Magufuli kwa kuzindua daraja la kigamboni jana tarehe 19 Aprili 2016. Blogu hii inakupongeza wewe binafsi kwa kuwa ndiye ulikuwa waziri wa ujenzi wakati mchakato wa ujenzi unaendelea. Hakika daraja hili ambalo umependekeza liitwe daraja la nyerere linakuwa kioo cha taifa na pia litachochea maendeleo eneo la kigamboni na Dar es Salaam kwa ujumla. Pia tunaipongeza shirika la hifadhi ya jamii NSSF chini ya uongozi wa aliyekuwa mtendaji mkuu wake aliyepita Dr Ramadhan Dau kwa kutoa baadhi ya fedha zilizowezesha ujenzi wa daraja hili. Pia blogu hii inaipongeza serikali ya Jakaya Kikwete kwa kutoa uamuzi wa ujenzi wa daraja hili.

Blogu hii inaomba daraja hili litunzwe na watu wote na wasimamizi wawe wakali kwa yeyote atakayehujumu miundombinu ya daraja hili. Blogu hii inasema hivi kutokana na baadhi ya watu wasiowaaminifu kuhujumu miundombinu ya barabara na madaraja kwa sababu mbalimbali kama uuzaji wa vyuma chakavu. 

Aidha blogu hii inaomba serikali kuendelea na juhudu ya ujenzi wa barabara na hasa za juu jijini Dar es Salaam na majiji mengine ili kuondoa kero ya msongamano wa magari. 

No comments:

Post a Comment