Wednesday, April 20, 2016

Hongera Serengeti Boys kwa kuwafunga mafarao wa Misri mara mbili

Picha: tanzaniatoday.com
Licha ya kuwa ilikuwa mechi ya kirafiki ya kimataifa, blogu hii inaipongeza timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 17 serengeti boys kwa kuifunga timu ya taifa ya Misri mara mbili. Hakika kila mtanzania anajua ubora wa timu za Misri na hivyo kiwango walichoonyesha vijana wetu wa kitanzania kinahitaji pongezi za dhati. Pia blogu hii inawapongeza makocha na benchi zima la ufundi kwa juhudu walizofanya na wanazoendelea kufanya. Pia tunaipongeza TFF kwa kuilea timu hii na kuwa na mafanikio haya. Blogu hii inaomba TFF na wadau wengine wa mpira wa miguu nchini na hasa wizara ya Elimu, Michezo na TAMISEMI kuunganisha nguvu na kuwa na mpango wa kuhakikisha michezo inachezwa na kushindaniwa kwenye shule zetu kiwilaya, kimkoa, kikanda na kitaifa. Kwa kufanya hivyo taifa litaweza kuwa na vijana wengi wenye vipaji na wanaojitambua maana watakuwa na ujuzi wa michezo na elimu ya darasani pia.

No comments:

Post a Comment