Picha:cctv-africa.com
Tumuunge mkono JPM kwa kuhakikisha kila mtanzania analipa kodi. Rais John Pombe Magufuli amejipambanua katika kuwaletea wananchi maendeleo. Katika juhudi zake hizo amewahimiza sana wananchi na hasa wafanyabiashara kulipa KODI. Nchi zote zilizopiga hatua kubwa ya maendeleo zinahakikisha kila mwananchi analipa kodi inayostahili.
Blogu hii imependa kauli ya Mh Rais isemayo "...ukiuza toa risiti....ukinunua dai risiti..." ili kodi irudi serikalini kwa ajili ya kuleta maendeleo kwa wananchi.
Aidha blogu hii inaomba Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kukusanya kodi kikamilifu na kuwashughulikia wale wote wanaokwepa kukwepa kodi. Aidha blogu hii inaishauri serikali kutafuta vyanzo vipya vya kupata mapato ambavyo havijaguswa.
....UKIUZA TOA RISITI....UKINUNUA DAI RISITI.....
No comments:
Post a Comment