Monday, January 2, 2017

Hongera JPM kwa kuliweka sawa sakata la kiwanda cha simenti cha DANGOTE

Tokeo la picha la magufuli
Picha: wikipedia

Hongera serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, chini ya Rais Mh Dr John Pombe Joseph Magufuli kwa kuliweka sawa sakata la kiwanda cha simenti cha DANGOTE. Kila mtu anajua mchango wa kiwanda hiki kikubwa nchini, na hasa kwa uzalishaji wake mkubwa wa simenti na upatikanaje wake kwa bei nafuu.

Blogu hii pia inampongeza Waziri wa Nishati na Madini Mh  Prof. Sospeter Muhongo na Waziri wa Viwanda na Biashara Mh Charles Mwijage kwa kuhakikisha sakata hili linaisha na kiwanda kinaendelea na uzalishaji. Kiwanda cha DANGOTE licha ya kuzalisha simenti kwa wingi na kwa bei nafuu pia kinasaidia kwa kiasi kikubwa ongezeko la ajira nchini.


Blogu hii imefurahi kwa jinsi viongozi wanavyoweza kuwalinda wawekezaji wakini kama DANGOTE. Hongera sana serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na hasa JPM.

No comments:

Post a Comment