HONGERA kipa wa KILIMANJARO stars IVO MAPUNDA. Katika mechi ya robo fainali ya kombe la challenge dhidi ya Timu ya Taifa ya Uganda, mlinda mlango huyo ambaye kwa sasa yupo nchini Kenya akidakia moja ya vilabu nchini humo ameonyesha umahili wa hali ya juu sana. Katika mechi hiyo ya robo fainali iliyofanyika jumamosi tarehe 7 disemba 2013, MAPUNDA aliokoa penati mbili ambazo ziliiwezesha Kilimanjaro stars kutinga Nusu Fainali. MAPUNDA alikuwa kipa namba moja wa Timu ya Taifa ya Tanzania miaka ya nyuma lakini baadae alitemwa!! Mwaka huu kocha wa Timu ya Taifa ya Bara alimjumuisha kwenye kikosi cha Kili stars.
Lakini MAPUNDA inaonekana sasa amerudi kwenye kiwango chake na ameonyesha uwezo na kujituma. Hakika blogu hii inampongeza MAPUNDA kwa kutupeleka NUSU FAINALI lakini pia kwa kulipigania TAIFA kwa umahili mkubwa. Kwa walioangalia mechi ile na zingine watakubaliana na blogu hii kuwa MAPUNDA alijituma sana na kuonyesha juhudi kubwa. Blogu hii inaomba wachezaji wengine wa kitanzania waonyeshe juhudi kama alivyoonyesha MAPUNDA. Kwa kucheza kwa juhudi kama alivyofanya MAPUNDA kunaweza kutufikisha mbali katika mashindano ya kimataifa.
Picha:footballzz.com
No comments:
Post a Comment