Friday, December 27, 2013

Waziri wa Elimu Dr Kawambwa amewaagiza Maafisa Elimu nchini kuhakikisha walimu wapya wanalipwa stahili zao mapema

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dr Shukuru Kawambwa amewaagiza Maafisa Elimu wa mikoa na wilaya nchini kuhakikisha walimu wapya wanalipwa stahili zao mapema. Aidha waziri huyo amewaagiza maafisa hao wa elimu kuhakikisha walimu wapya wanapokelewa vizuri katika maeneo yao ya kazi.


Blogu hii inapenda kumpongeza Waziri Dr Kawambwa kwa kauli hiyo ya kuwataka maafisa elimu nchini kuhakikisha walimu wapya wengi wao wakiwa walimu vijana kulipwa stahili zao mapema. Hii itawafanya walimu hao wapya wasikatishwe tamaa ya kukaa katika vituo vyao walipopangiwa. Pia kuwajali walimu hasa wanapoajiriwa kwa mara ya kwanza inakuwa kama motisha kwao. Aidha Waziri amewaagiza maafisa hao kuhakikisha kuwa wanafuatilia suala zima la ufundishaji mashuleni na kuwa na walimu wakuu wenye sifa. 


Aidha blogu hii inaomba, wizara ya elimu kwa kushirikiana na TAMISEMI kufuatilia kwa karibu ili kuhakikisha walimu hao wapya wanapokelewa vizuri na wanahudumiwa ipasavyo. Ni vyema kukawa na ufuatiliaji wa karibu katika kuhakikisha walimu wanapatiwa mahitaji yao ya lazima na hasa kwa hawa wlimu wapya.


Duniani kote mwalimu ni nguzo ya Taifa na hakuna maendeleo bila elimu bora na elimu bora inatoka kwa mwalimu aliyeandaliwa na kuhudumiwa vizuri. Kwa habari zaidi soma majira


Picha: 24tanzania

No comments:

Post a Comment