Sunday, December 8, 2013

Tuige siasa za Komredi MANDELA kumuenzi _ aliwaunganisha watu wote bila ya kubeza wengine!

Hakika Kifo cha Komredi Nelson Mandela wenyewe wanamwita MADIBA kimetikisa dunia hasa Tanzania. Kiongozi huyu tunaweza kusema ni wa kufikirika! Alipinga ubaguzi wa rangi dhidi ya utawala wa makaburu kule Afrika ya Kusini. Alifungwa zaidi ya miaka 27 na kuteswa sana. Licha ya mateso hayo alizidi kuwa mtetezi wa wanyonge akiwa gerezani na kukataa msamaha wenye masharti.

Baada ya kutolewa gerezani miaka ya tisini alichaguliwa kuwa Rais wa kwanza mweusi katika utawala wa kidemokrasia nchini Afrika ya Kusini. Kikubwa ambacho wengi KINATUSHINDA! ni kuwa aliwasamehe wote waliomkosea wakati wa UBAGUZI WA RANGI!! Aliwasihi waafrika weusi WASILIPIZE KISASI dhidi ya wazungu! Aliwahimiza WAAFRIKA weusi wasiwabeze na kuwasimanga WAZUNGU ila washirikiane kujenga TAIFA JIPYA. 

Mandela aliamini adui alikuwa ni ubaguzi wa RANGI!!! na sio RANGI ya MTU!! Kibinadamu sio rahisi kusamehe watu waliokupa mateso makali. Mandela aliepusha mauaji ya kisasi dhidi ya wazungu. Kama angekuwa kiongozi wa visasi, Afrika Kusini kungekuwa na mauaji ya kutisha dhidi ya watu weupe. Hii ingetokana na waafrika weusi kulipiza kisasi na kuwabeza weupe!! Mandela alikataa hayo yote na kuchukuliwa wananchi wote wa Afrika ya Kusini kama kitu kimoja bila kujali RANGI ya MTU!! Hakika Dunia itamkumbuka sana Mandela!

Blogu hii inaomba hulka, tabia na mwenendo wa MANDELA uigwe na VIONGOZI wa sasa ndani ya DUNIA hii ambayo tupo kwa MUDA tu. Blogu hii inaomba siasa za kubezana, za visasi na zisizo na tija kuepukwa na viongozi na watu wote. Lengo kwa wote ni kuleta maendeleo na sio kubezana na siasa zisizo msaidia mtu wa kawaida. Ukiangalia MANDELA hakuwahi hata siku moja kufurahia udhaifu wa wengine mara baada ya kuwa RAIS wa Afrika Kusini ila aliwashika mkono hata wale walioaminika kuwa walikuwa maadui zake enzi za ubaguzi wa RANGI.

Hakika, MANDELA ni SOMO kubwa kwa WAAFRIKA, katika kuleta ustawi na maendeleo ya kistaarabu ya bara hili lenye migogoro isiyo na tija.

R.I.P MANDELA!! MWENYEZI MUNGU UIWEKE ROHO YAKE MAHALA PEMA PEPONI AMINA!!!
Picha:consortiumnews.com

No comments:

Post a Comment