Hongera serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kwa kutoa sera ya gesi ya mwaka 2013. Sera hii imeeleza wazi kuwa gesi ni mali ya taifa na inapaswa kuwanufaisha wananchi na pia itauzwa nje ya nchi pale tu mahitaji ya ndani yatapotimizwa. Sera hiyo imeainisha kuwa ni lazima serikali na wananchi wanufaike na rasilimali hiyo na pia kunakuwa na haki na usawa kwa wadau katika uvunaji na utumiaji wa rasilimali hiyo. Sera hiyo imesisitiza kujenga mifumo ya kitaasisi, miundombinu na nguvu kazi ya kuhudumia na kuendeleza sekta ya gesi nchini.
Hakika blogu hii inaipongeza sana serikali pamoja na wadau wengine kwa kufanikisha sera hii muhimu kwa taifa. Ni wakati muafaka kwa wadau na wananchi kuchangamkia fursa itakayotokana na uchimbaji na usambazaji wa gesi nchini. Ni matumaini ya blogu hii kuwa uchimbaji na usambazaji wa gesi utanufaisha taifa na kuinua uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa jumla.
Photo:dullonet.com
Photo:dewjiblog.com
No comments:
Post a Comment