Watanzania tuache siasa za maji taka!!!Tujadili hoja za msingi zilizo mbele yetu kama vile elimu, katiba, madini, maliasili, upatikanaji wa maji na umeme nk. Tuache ushabiki wa uNCCR, uCUF, uCCM, uUDP, uCHADEMA nk!!! Tuache kudharirisha watu bila sababu za msingi. Kumbukeni JK ni RAIS tupende au tusipenda! kumdhihaki si jambo zuri hata kidogo. Twende kwenye hoja ya msingi kama mtanzania mmoja mmoja!! kuitana majuha haisaidii. Nitawapa mfano, JK ameonyesha ukomavu wa hali ya juu wa kisiasa, ameweza kukutana na makundi mbalimbali ya jamii na kisiasa na kusikiliza maoni yao. Hakika JK amewafunda wanasiasa wa Tz kuwa siasa sio fitna, matusi ama kubeza mawazo ya mwenzio bali siasa ni maridhiano, maelewano, upendo, maendeleo, amani bila ya kudharau maoni ya watu hata kama ni wengi ama wachache!! Watanzania hasa vijana badilikeni ili nchi yetu iweze kupiga hatua ya maendeleo. Mimi nimefurahi wakati JK anahutubia bunge majuzi Mwenyekiti na Mkuu wa kambi ya upinzani bungeni alikuwa akipiga makofi mara kwa mara wakati JK alipokuwa anahutubia. Upigaji makofi ule umeonyesha hata wapinzani wanaunga mkono hoja zinazotolewa na upande wa pili wa shilingi hata kama mtoa hoja yuko chama tawala ama chama kingine! Hali hii ndio watanzania wanayohitaji. Tujadili hoja za msingi kwa watanzania na watanzania watawaunga mkono viongozi hao bila kujali wanatoka upande gani wa shilingi. JK bila kumugunya maneno ameonyesha weledi, ustaarabu, uungwana na ukomavu wa hali ya juu, amejali maslahi ya watanzania wote bila ubaguzi, nendeni youtube ama kwenye mitandao ya kijamii kuangalia hotuba yake hiyo aliyoitoa bungeni hivi karibuni Dodoma. Hakika JK amekuwa kama mwalimu JKN!! Sasa na sisi tufuate nyayo zake na tuache siasa za kuchafuana ambazo hazitatufikisha popote. Tanzania tunataka maendeleo ya kweli na sio malumbano yasiyo na tija. Tanzania kwanza, ubinafsi nyuma!
No comments:
Post a Comment