Monday, November 11, 2013

Rais UHURU KENYATTA wa KENYA asema KENYA iko tayari kushirikiana na Tanzania

Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya kupitia waziri wa mambo ya nje wa nchi hiyo, Mh. Amina Mohamed, ametuma salamu akisema kuwa nchi ya Kenya iko tayari kushirikiana na Tanzania. Hata hivyo, Rais wa Kenya amesema kwamba  walijiingiza katika mazungumzo na Uganda pamoja na Rwanda kuhusu ujenzi wa bomba la mafuta na reli bila kufahamu kwamba ilikuwa inavunja misingi iliyowekwa na jumuiya hiyo.
 
Hakika hatua hii ya kistaarabu ni ya kipekee na inastahili kupokelewa kwa mikono miwili na watanzania pamoja na Rais wetu JK. Yalizungumzwa mengi, kabla ya Rais Kenyatta kutoa msimamo huo kupitia waziri wake wa mambo ya nje.
 
Blogu hii inaamini kuwa UMOJA NI NGUVU! NA UTENGANO NI UDHAIFU. Ikumbukwe, Tanzania ni sehemu ya AFRIKA MASHARIKI kijiografia, kihistoria, kiasili na pia itakuwa kosa kubwa sana kujitoa!. Ni furaha ya blogu hii kuwa kweli JK alizungumza vitu vya kweli vilivyotokea kabla. Hii inadhibitishwa na kauli ya UHURU na sasa angalau mambo yatakuwa shwari. AFRIKA MASHARIKI IDUMU!
 
Picha: mwananchi -  Mh. Bernard Membe (waziri wa mambo ya nje wa Tanzania) na Mh. Amina Mohammed (waziri wa mambo ya nje wa Kenya)

No comments:

Post a Comment