Wednesday, December 10, 2014

Hongera Idris Sultan kwa kujizolea kitika, takriban milioni 500 za kitanzania toka shindano la Big Brother Hotshots nchini Afrika Kusini

Hongera Idris Sultan kwa kujizolea kitika, takriban milioni 500 za kitanzania. Blogu hii imefurahishwa na ushindi huu ulioupata toka BBA katika shindano la Big Brother Hotshots nchini Afrika Kusini. Ushindi huu si wa Idris pekee bali ni ushindi wa watanzania wote. Ushindi huu pia unawafundisha vijana wengine wa kitanzania katika nyanja zote za michezo, sanaa na muziki kuwa inawezekana kupata ushindi. Blogu hii inaomba vijana wengine katika nyanja zote waige mfano wa kujituma bila ya kukata tamaa kama alivyoonyesha Idris katika shindano hili. Hongera sana Idris. Kwa habari zaidi bofya

Picha:bigbrotherafrica


No comments:

Post a Comment