Sunday, December 14, 2014

WANAWAKE WANAWEZA!!!! Hongera Jonisia Rukyaa kwa kuwa mwanamke wa kwanza kuchezesha MECHI kubwa ya SIMBA na YANGA ya NANI MTANI JEMBE 2

Hongera mwanamama (Jonisia Rukyaa) toka mkoa wa Kagera kwa kuwa mwanamke wa kwanza nchini Tanzania kuchezesha mechi kubwa ya watani wa jadi, Simba Sports Club (Simba) na Young Africans Sports Club (Yanga) kupitia shindano la Bia ya Kilimanjaro ya NANI MTANI JEMBE 2. Katika mechi hiyo iliyofanyika jana (jumamosi, 13/12/2014) jijini Dar es Salaam katika uwanja wa Taifa, ambapo SIMBA waliibuka na ushindi wa mabao 2 kwa 0. Blogu hii inaomba wanawake wengine wajitokeze katika nyanja mbalimbali hususan michezo ili kufuata nyayo za mwanamama huyu hodari.

Hakika blogu hii inakupongeza sana licha ya changamoto chache zilizojitokeza ambazo hata upande wa waliopoteza (YANGA) wanazikubali. Blogu hii inakuomba utafute mkanda wa mechi ile na uondoe makosa machache ambayo WOTE tuliyaona. Ila kwa kiasi kikubwa ulijitahidi sana. Big UP mwanamama, Kweli WANAWAKE wanaweza!! Tembelea michuzi ujionee picha za mchezo huo muhimu.

Picha: Michuzi blog

No comments:

Post a Comment