Monday, December 1, 2014

Hongera Bodi ya Utalii kwa kutangaza vivutio vya utalii vyaTanzania kupitia Ligi Kuu ya Uingereza

Picha:tanzaniatoday.co.tz

Hongera Bodi ya Utalii ya Tanzania kwa kutangaza vivutio vya utalii kupitia ligi maarufu duniani, Ligi Kuu ya Uingereza. Kila mmoja wetu anajua umaarufu wa Ligi hii duniani. Ni ligi inayofuatiliwa na kutazamwa na watu wengi sana duniani kupitia njia mbalimbali ikiwemo matangazo ya Luninga. Katika mechi kati ya Sunderland na Chelsea ambapo wachezaji wa Sunderland walivalia jezi za mazoezi (T-shirts) zilizokuwa na tangazo “Visit Tanzania” Mechi hiyo iliyofanyika nchini Uingereza iliishia kwa timu hizo kutoka suluhu ya bila kufungana. Ni matumaini ya blogu hii watu wengi walitazama tangazo hilo na hata kumbukumbu kubaki katika mitandao mbalimbali duniani. 

Hakika hili ni jambo zuri kwa maana lina mchango mkubwa katika kuinua uchumi wa taifa kupitia utalii. Tanzania ni nchi yenye vivutio vingi vya utalii ikiwemo Mbuga ya Serengeti, Mikumi, Ngorongoro, Mlima Kilimanjaro, vivutio vya Zanzibar na Bagamoyo nk. Kupitia Tangazo hili nchi yetu itatembelewa na watalii wengi zaidi na kuchangia pato la mtu mmoja mmoja na taifa kwa jumla.

Blogu inaipongeza serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kupitia kwa Rais Jakaya Kikwete kwa kuitangaza Tanzania. Vile vile Bodi ya Utalii pamoja na Wizara husika zinastahili pongezi za dhati. Juhudi hizi zinapaswa kuendelezwa. Blogu hii inaishauri serikali kwa kuwa kuna uwezekano mkubwa wa kuongezeka kwa abiria (watalii) kupitia viwanja vyetu vya ndege, hivyo ni wakati muafaka wa kiviboresha zaidi na kuwa na hadhi na mahitaji ya kimataifa. Blogu hii inatambua upanuzi wa kiwanja cha Mwalimu Julius Nyerere cha Dar es Salaam, hata hivyo viwanja vingine hasa Kilimanjaro, Mwanza na Zanzibar vinapaswa kuboreshwa ili kupokea wingi wa watalii na wageni toka nje ya nchi.

Kwa habari zaidi tembelea Tanzania tourist board  uone vivutio vilivyoko Tanzania.

No comments:

Post a Comment