Sunday, November 30, 2014

Pole na karibu Rais Mh Jakaya Mrisho Kikwete toka nchini Marekani

jk3
Picha:dewjiblog.com

Blogu hii inapenda kukupa pole Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Jakaya Mrisho Kikwete kwa kurudi salama Tanzania toka Marekani ulipokuwa unashughulikia afya yako. Afya yako ni afya ya watanzania wote. Blogu hii imeona ni busara kukupa pole kwa niaba ya watanzania na kukukaribisha tena ili kuzidi kuwaletea maendeleo wananchi.


Blogu hii imefurahishwa na ujasiri wa kuelezea afya yako kwa wananchi siku ya Jumamosi tarehe 29 mwaka 2014 ulipowasili toka nchini Marekani. Hakika umetufundisha somo la kupima afya zetu mara kwa mara ili kubaini tatizo mapema. Somo hili hasa la kupima afya mara kwa mara ni muhimu ukizingatia watanzania kutokuwa na utamaduni huo hata kama kuna fursa ya huduma za afya.  Pole sana Rais wetu na karibu nchini uzidi kuwaletea wananchi maendeleo.

No comments:

Post a Comment