Sunday, November 30, 2014

Hongera Mh Mizengo Pinda kwa busara, subira na uvumilivu wakati wa mjadala wa sakata la Tegeta ESCROW ndani ya Bunge

Image result for pinda mizengo
Kwa namna ya pekee blogu hii inampongeza Waziri Mkuu “mtoto wa mkulima” Mh. Mizengo Pinda kwa busara, heshima, ustahimilifu na subira juu ya Sakata la “account” ya Tegeta ESCROW. Hakika umetufundisha kitu katika sakata hili na kudhihilisha kuwa uongozi ni kujali maslahi mapana ya wananchi na siyo vinginevyo. 

Blogu hii inakupongeza kwa jinsi ulivyotoa maneno ya kuwaunganisha watanzania wakati wa kufunga Bunge jumamosi tarehe 29 mwaka 2014. Ustahimilifu, subira, heshima, busara uliyoonyesha ni SIFA ya KIONGOZI MKUU. Hakika SIFA hizo unazo. Pia blogu hii imependa kauli zako ikiwemo “Yaliyopita si ndwele tungange na yajayo”, ni kauli nzuri kwa ustawi wa taifa lolote.

Ni matumaini ya blogu hii na watanzania kuwa mapendekezo ya wabunge wetu wote juu ya sakata hili yatafanyiwa kazi kwa uadilifu na uaminifu mkubwa chini ya UONGOZI WAKO. Blogu hii imejionea kuwa kauli zako katika suala hili ni za kuwaunganisha watanzania. Aidha ahadi ulizotoa zimewafuta machozi watanzania wote bila kujali itikadi zao.

No comments:

Post a Comment