Kwa namna ya pekee blogu hii inampongeza Waziri Mkuu “mtoto wa mkulima”
Mh. Mizengo Pinda kwa busara, heshima, ustahimilifu na subira juu ya Sakata la
“account” ya Tegeta ESCROW. Hakika umetufundisha kitu katika sakata hili na
kudhihilisha kuwa uongozi ni kujali maslahi mapana ya wananchi na siyo
vinginevyo.
Blogu hii inakupongeza kwa jinsi ulivyotoa maneno ya kuwaunganisha
watanzania wakati wa kufunga Bunge jumamosi tarehe 29 mwaka 2014. Ustahimilifu,
subira, heshima, busara uliyoonyesha ni SIFA ya KIONGOZI MKUU. Hakika SIFA hizo unazo. Pia blogu hii
imependa kauli zako ikiwemo “Yaliyopita si ndwele tungange na yajayo”, ni kauli nzuri kwa ustawi wa taifa lolote.
Ni matumaini ya blogu hii na watanzania kuwa mapendekezo ya wabunge wetu
wote juu ya sakata hili yatafanyiwa kazi kwa uadilifu na uaminifu mkubwa chini
ya UONGOZI WAKO. Blogu hii imejionea kuwa kauli zako katika suala hili ni za
kuwaunganisha watanzania. Aidha ahadi ulizotoa zimewafuta machozi watanzania
wote bila kujali itikadi zao.
No comments:
Post a Comment