Sunday, November 30, 2014

Hongera kamati ya PAC chini ya Mh Zitto na Mh Filikunjombe juu ya sakata la Tegeta ESCROW

Image result for zitto kabweImage result for filikunjombe
Hongera Mh. Zitto Kabwe na Mh. Deo Filikunjombe pamoja na wajumbe wote wa kamati ya “PAC”. Hakika mmewatendea haki watanzania katika kipindi chote cha uchunguzi, uchambuzi na uwasilishwaji wa maadhimio yaliyohitimishwa Jumamosi tarehe 29 mwaka 2014. 

Sakata la “account” ya Tegeta ESCROW halikuwa jambo dogo. Uimara na umahili wenu kwa kusaidiana na wajumbe wote wa PAC umewafuta machozi watanzania bila kujali itikadi ya vyama. Kamati yenu, imetukumbusha kuwa “cheo ni dhamana”, imetukumbusha “cheo siyo dharau”, imetukumbusha “uongozi ni uadilifu, ukweli, kutenda haki na uaminifu.  

Kazi yenu imeleta heshima ya nchi yetu, na kurudisha imani kwa watanzania kupitia wawakilishi wao. Aidha mmesaidia kuokoa rasilimali za nchi hii kwa wakati huu na kwa miaka ijayo, mmedumisha nidhamu kwa wote hususan watendaji na viongozi. 

Blogu hii inawapongeza sana, Mwenyezi Mungu Awabariki Sana. Blogu hii inapendekeza nchi yetu itilie mkazo suala la MAADILI siyo kwa viongozi wa umma pekee ila hata kwa watendaji wote ikiwemo sekta binafsi. 

Kuwepo na vyombo vya kuhakikisha nidhamu inakuwepo kwa watu wote. Blogu hii inafurahi uwepo wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa “PCCB”, Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali “CAG”, Ofisi ya Maadili nk. Blogu hii inaomba vyombo hivi vipewe nguvu na nyenzo zaidi kikatiba ili kulinda maslahi ya Taifa letu. Kazi ya kwanza kwa vyombo hivi na vingine ikiwemo Polisi, Usalama wa Taifa ni kulinda maslahi ya nchi yetu ikiwemo ya kiuchumi pamoja na rasilimali za nchi. 

Kuna haja ya vyombo hivi na vingine vikafanya kazi kwa ushirikiano ili kuleta ufanisi wa kimaadili, usalama na uzalendo. Suala la usalama ni pamoja na ulinzi wa rasilimali za Taifa ikiwemo pesa za serikali na walipa kodi. 

No comments:

Post a Comment