Sunday, November 30, 2014

Hongera wabunge wote wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kusimamia sakata la Tegeta ESCROW

Picha: thehabari.com

Hongera wabunge wote wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa jinsi mlivyosimamia suala zito la Sakata la “account” ya Tegeta ESCROW. Blogu hii inaamini suala hili lilikuwa nyeti, gumu na lililokuwa linagusa nyoyo za watanzania. Ni suala ambalo lilikuwa na majibu mawili moja kujenga ama kubomoa taifa. Hakika wabunge wote mmerudisha imani kwa wananchi wa nchi hii kwa kuweka mbele maslahi mapana ya nchi yetu. Wabunge mmetukumbusha kuwa uongozi ni dhamana, uongozi ni uadilifu, uongozi ni uwajibikaji, uongozi ni ukweli. Kiongozi asiye mkweli ni tatizo, kiongozi asiye mwadilifu ni tatizo. 

Blogu hii inaomba kuwataja wabunge wachache kwa niaba ya wabunge wote kwa jinsi walivyosaidia kuwatetea na kuwaunganisha watanzania, Mh Zitto Zuberi Kabwe, Mh Deo Filikunjombe, Mh Mwigulu Nchemba, Mh David Kafulila, Mh James Mbatia, Mh Ole Sendeka, Mh Dr Hamisi Kingwangala, Mh William Lukuvi, Mh Freeman Mbowe, Mh Kangi Lugola, Mh Stephen Wasira, Mh John Mnyika nk.  

Blogu hii inaomba mwelekeo huu uendelee hata katika masuala mengine ya kitaifa, na bila kusahau wajibu wenu wa kuwawakilisha wananchi na kuisimamia serikali ili ilete maendeleo ya kweli kwa wananchi wake. Hakika siku ya Jumamosi tarehe 29 mwaka 2014 ni siku ya kukumbukwa kwa taifa letu. Mwenyezi MUNGU awabariki WABUNGE wote wa BUNGE hili kwa kutenda HAKI na KUWABEBA WATANZANIA.

No comments:

Post a Comment