Saturday, March 7, 2015

Asante Mh. Dr. Magufuli kwa kumfagilia Mh. Mbowe na kuonyesha kuwa siasa sio chuki bali ni maendeleo

Picha:mwananchi.co.tz

Asante sana mpiganaji, mchapakazi na mzalendo wa kweli Mh Dr. John Pombe Magufuli kwa kuwafundisha wananchi wa Tanzania kuwa siasa sio chuki wala ugomvi. Siasa ni kuwa na mitazamo tofauti yenye nia moja ya kuwaletea wananchi maendeleo na si vinginevyo. Mh Dr. Magufuli alimtaja kiongozi wa kambi ya upinzani Bungeni Mh. Freeman Mbowe (Mbunge wa Hai) kuwa ni kiongozi anayefuatilia maendeleo ya watu wake bila ya kujali itikadi za kisiasa. Mh Dr. Magufuli aliyasema hayo kwenye mkutano wa hadhara mara baada ya kukagua ujenzi wa barabara inayotoka Kwasadala kupitia Masama mpaka Machame hivi karibuni.

Blogu hii inampongeza sana Mh Dr. Magufuli kwa kauli yake nzuri inayoleta umoja na amani ya kweli kwa watanzania. Blogu hii inawaomba wanasiasa wengine kuiga mwenendo huu kwani mitazamo tofauti ya siasa sio nongwa! Tuepuke watu wanaopenda kuona taifa hili ama viongozi wa kisiasa wakikinzana bila sababu ya msingi.

Kwa habari zaidi soma mwananchi.


No comments:

Post a Comment