
Picha: tanzaniatoday.co.tz
Hakuna kama Azam Tv. Jana tarehe 06 mwezi 03 mwaka 2015 itakuwa siku ya kukumbukwa katika sekta ya habari ya nchini Tanzania mara baada ya kituo cha Azam Tv kuzindua studio mpya ya kisasa yenye thamani ya dola za kimarekani milioni 31 (zaidi ya bilioni 56 za kitanzania).
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dr. Jakaya Kikwete ndiye alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo na ndiye aliyekata utepe akiambatana na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mh. Dr Fenella Mukangara sambamba na viongozi na wafanyakazi wa Azam Tv Tabata Relini jijini Dar es salaam.
Hakika blogu hii inaipongeza sana Azam Tv hususan wamiliki na uongozi wake kwa ujumla kwa juhudi za dhati za kuboresha sekta ya habari nchini. Kituo hiki ambacho kina mwaka mmoja toka kianzishwe kimepiga hatua kubwa sana. Moja ya hatua kubwa ambayo kila mtanzania anaiona ni kuonyesha "live" ligi mbalimbali za michezo ikiwemo Ligi Kuu ya Vodacom. Blogu hii inaamini Azam Tv itakuwa na ubora kama vituo vingine vya kimataifa kama vile BBC, CNN SKY nk. SISI ni Azam Tv wewe je?
No comments:
Post a Comment