Uzinduzi wa treni ya mizigo toka Dar es Salaam kwenda nchi jirani hususan Rwanda ni jambo jema sana kwa ustawi wa nchi za maziwa makuu na ukanda wa Afrika Mashariki. Aidha uzinduzi wa treni ya mizigo mbali na kupunguza gharama kubwa za usafirishaji pia zitapunguza kwa kiasi kikubwa muda unaopotea njiani kutokana na vikwazo mbalimbali barabarani. Pia uzinduzi huu utapunguza usumbufu usiokuwa wa lazima.
Blogu hii inaipongeza sana serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya uongozi wa Dr Jakaya Mrisho Kikwete kwa kutimiza lengo muhimu sana kwa uchumi wa Tanzania na nchi jirani. Hakika haya ndiyo maendeleo wananchi wanayoyataka.
Blogu hii inaomba serikali ijikite zaidi kuhakikisha kuna kuwa na usafiri wa treni kila siku kwa ajili ya kusafirisha mizigo na abiria toka Dar es Salaam kwenda mikoani na nchi jirani. Usafiri wa treni duniani kote ni usafiri wenye usalama na gharama nafuu ukilinganisha na usafiri wa mabasi. Aidha blogu hii inaomba serikali iwekeze katika usafiri wa reli ndani ya majiji kama vile Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya, Tanga na Arusha ili kukabiliana na msongamano wa magari barabarani.
Kwa habari zaidi tembelea wavuti
Kwa habari zaidi tembelea wavuti
Rais Kagame akinyanyua bendera kuashiria uzinduzi wa Treni ya Mizigo
toka Dar es Salaam kwenda Rwanda (http://www.wavuti.com)
No comments:
Post a Comment