
Picha:blog.ikulu.go.tz
Hongera Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete "JK" kwa kuwajali na kuwathamini wasanii nchini Tanzania. Sekta ya usanii hapo zamani ilikuwa inaonekana ni sekta ya kibabaishaji, lakini sasa imekuwa sekta rasmi inayochangia uchumi wa nchi yetu. JK umejitahidi kuwainua na kuwatambua wasanii wetu. Tunaomba Rais ajaye afuate nyayo zako ili sekta hii itoe mchango mkubwa kwa uchumi wa taifa letu.
Blogu hii imefurahishwa sana kwa Rais kujumuika na wasanii siku ya alhamisi tarehe 6 mwezi wa 8 mwaka 2015. JK umekuwa shujaa wa wasanii nchini. Asante wasanii kwa kazi njema za kuwaburudisha watanzania, asante NIKI WA PILI kwa hotuba yako nzuri, hakika uko juu sana. Asante JK kwa kukubali kuwa mlezi wa wasanii.
Blogu hii inaomba serikali kuweka mikakati dhabiti katika ulinzi wa biashara za wasanii na ulinzi wa maisha ya msanii mmoja mmoja na haki zao. Mfano, wasanii wanaweza kuingizwa kwenye bima za afya na bima nyinginezo kupitia "shows" zao. Na hii inawezekana, serikali ijayo ifanye hayo.
No comments:
Post a Comment