
Picha:en.wikipedia.org
Hongera Azam FC kwa kuchukua ubingwa, Kombe la Klabu Bingwa Afrika Mashariki lijulikanalo kama "Kombe la Kagame" Jumapili (02/08/2015) kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Ushindi wa Goli 2 - 0 dhidi ya Gor Mahia ya Kenya ni mkubwa na umewafurahisha sana watanzania na kuwaondolea unyonge. Blogu hii imefurahishwa na juhudi ya timu hii pamoja na benchi lake la ufundi na manejimenti kwa ujumla. Jambo zuri sana ni kuwa timu hii katika mashindano haya haijafungwa goli lolote ndani ya dakika dk 90 katika michezo yake yote.
Hakika kikosi hiki kilichochukua ubingwa hakita sahaulika:
Hakika kikosi hiki kilichochukua ubingwa hakita sahaulika:
- Aishi Manula
- Shomari Kapombe
- Said Morrad
- Aggrey Morris
- Serge Wawa
- Mugiraneza Jean Baptiste
- Himid Mao
- Kipre Tchetche/Kavumbagu
- Ame Ally/Frank Domayo
- John Bocco
- Farid Mussa/ Erasto Nyoni
Blogu hii inajua kuwa timu ya Azam FC ina mfumo mzuri, ina uwanja wake, ina vifaa vya michezo vya uhakika, inalea vijana wadogo nk. Vitu hivi ndio chachu kubwa ya ubingwa wao wa Kagame. Blogu hii inaomba juhudi hizi za Azam FC ziendelee hata kwenye kombe la washindi barani Afrika ili jina la Tanzania lizidi kupaa.Hakuna kama Azam FC Tanzania!!
Kwa habari zaidi tembelea Azam FC
No comments:
Post a Comment