
Picha:en.wikipedia.org
Hongera sana Diamond Platnumz kwa ushindi ulioupata barani Afrika. Katika Tuzo zilizotolewa na kituo cha Television cha MTV nchini Afrika Kusini, msanii wa Tanzania Diamond ameshida kwa kishindo tuzo ya mtumbuizaji bora barani Afrika "Best Live Act" kupitia shindano la MTV (MAMA'S) Africa Music Awards 2015. Shindano hilo lilifanyika ndani ya ukumbi Durban International Convention Center (ICC) nchini Afrika Kusini 19 Julai 2015.
Blogu hii imefurahishwa na ushindi wa msanii huyu wa Tanzania na imemwomba azidi kupambana na kupiga hatua zaidi kimataifa. Pia blogu hii inawaomba wasanii wengine wa Tanzania kuiga na kufuata nyayo za Diamond ili wapate mafanikio. Blogu hii inaomba watanzania wakiwemo wadau wote wa muziki nchini kuwa wakweli katika upatikanaji wa washindi katika tuzo mbalimbali ili kusaidia kuibua na kukuza vipaji na sio kuvidumaza.
Hakunaga kama Diamond Platnumz.
No comments:
Post a Comment