Monday, July 13, 2015

Hongera Mh Samia Suluhu Hassan kwa kuteuliwa kuwa Mgombea Mwenza kupitia CCM

Picha:tanzaniatoday.co.tz

Hakika wanawake wanaweza! Hongera Mh Samia Suluhu Hassan kwa kuteuliwa kuwa Mgombea Mwenza wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM). Kuchaguliwa kwako kumeonyesha kuwa wanawake wanaweza kuongoza ngazi yoyote ya uongozi nchini Tanzania. Jana jumapili ya tarehe 12 mwezi wa 07 mwaka 2015 mjini Dodoma ilikuwa siku ya kukumbukwa na watanzania na hasa wakinamama nchini.

Kitendo hiki kimetoa hamasa kubwa kwa wanawake wengi nchini Tanzania kujiamini kuwa wanaweza. Blogu hii inaomba wanawake wazidi kujitokeza katika kuwania nafasi za maamuzi na kisiasa nchini Tanzania kupitia uchaguzi mkuu utakaofanyia oktoba mwaka huu 2015.


Hakika wanawake wanaweza!

No comments:

Post a Comment