
Picha: un.org
Hakika wanawake wanaweza! Hongera
Balozi Amina Salum Ali na Dr Asha-Rose Mtengeti Migiro kwa kuonyesha kuwa
wanawake wanaweza. Kufika kwenu kwenye TATU BORA ya kutafuta mgombea urasi kwa
tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)
kumeonyesha kweli na kwa hakika wanawake nchini Tanzania wana uwezo mkubwa sana
katika ngazi za maamuzi. Wakina mama hawa walifika tatu bora jumamosi tarehe 11/07/2015 mjini Dodoma pamoja na Mh John Pombe Magufuli.
Tendo mlilofanya limetoa hamasa
kwa wanawake wengine nchini kujiamini. Ni matarajio ya blogu hii kuwa kwa
kufuata nyayo za wakina mama hawa (Balozi Amina Salum Ali na Dr Asha-Rose
Mtengeti Migiro), wanawake wengi sana nchini watajitokeza katika kuomba nafasi
za udiwani, ubunge na uwakilishi kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 2015. Blogu hii inaamini,
ili taifa hili liwe na ustawi unaostahili wanawake wanapaswa kushiriki
kikamilifu katika ngazi za maamuzi na kisiasa.
Ombi la blogu hii ni kwa wapiga kura wanawake
na wanaume kuwapigia kura za ndio MAMA zetu. Hakika NANI KAMA MAMA.
HAKUNA.....

Picha:cctv-africa
No comments:
Post a Comment