Wednesday, July 15, 2015

Hongera Azam TV kwa kuwa na mpango wa kuonyesha ligi kuu ya Hispania "La Liga" mwaka huu


Picha:sundayshomari.com

Hongera Azam TV kwa kuwa na mpango wa kuonyesha ligi kuu ya Hispania "La Liga" mwezi wa 8 mwaka 2015. Hayo yamesemwa na Mtendaji Mkuu wa Uhai Production Dunstan Tido Mhando jana tarehe 14 mwezi wa 7 mwaka huu kupitia Azam two ya Azam TV. Blogu hii imefurahishwa na hatua nzuri ambayo itatoa burudani kabambe kwa wana wa Afrika Mashariki na hasa wapenzi wa soka. 

Ni matarajio ya blogu hii kuwa kuwepo na maonyesho ya ligi kubwa duniani kutaenda sambamba na unafuu wa bei ili kuwawezesha watu wengi kuona burudani hii majumbani mwao.

Blogu hii inawaomba watu wazidi kujiunga na Azam TV ili izidi kutupa burudani na habari kwa uhakika na kwa bei nafuu. Hakika hakuna kama Azam TV katika Ukanda wa Afrika Mashariki.

No comments:

Post a Comment